MENU

Saturday, June 16, 2012

Miss Tanzania kupatikana leo

MREMBO bora wa Tanzania atakayekwenda kuiwakilisha nchi kwenye mashindano ya urembo dunia, anatarajia kujulikana leo katika shindano litakalofanyika kwenye Ukumbi wa 327, Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Shindnao hilo la dunia linatarajia kufanyika Agosti 18 nchini China.
Warembo 10 wanatarajia kujipanga ukumbini kuwania kushinda taji hilo na baadaye kuwaikilisha nchi kwenye mashindano ya urembo ya dunia.
Mratibu wa Shindano hilo, Hashim Lundenga aliiambia Mwananchi maandalizi kuwa, maandalizi yote yamekamilika na mshindi atajinyakulia Sh2 milioni.
"Unajua shidano la dunia hufanyika kila mwaka mwezi Oktoba, lakini kwa sasa linafanyika mapema zaidi kutokana na mabadiliko ya kalenda," alisema Lundenga.
Walimbwende watakaopanda jukwaani leo ni pamoja na Pendo Laiser, Lisa Jensen, Christine Willium, Jenifer Kakolaki, Gloryblanca Mayowa, Hamis Hasan, Queen Saleh, Mwajabu Juma, Neema Saleh na Stela Mbuge.