MREMBO bora wa Tanzania atakayekwenda kuiwakilisha nchi kwenye
mashindano ya urembo dunia, anatarajia kujulikana leo katika shindano
litakalofanyika kwenye Ukumbi wa 327, Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Shindnao hilo la dunia linatarajia kufanyika Agosti 18 nchini China.
Warembo
10 wanatarajia kujipanga ukumbini kuwania kushinda taji hilo na baadaye
kuwaikilisha nchi kwenye mashindano ya urembo ya dunia.
Mratibu
wa Shindano hilo, Hashim Lundenga aliiambia Mwananchi maandalizi kuwa,
maandalizi yote yamekamilika na mshindi atajinyakulia Sh2 milioni.
"Unajua
shidano la dunia hufanyika kila mwaka mwezi Oktoba, lakini kwa sasa
linafanyika mapema zaidi kutokana na mabadiliko ya kalenda," alisema
Lundenga.
Walimbwende watakaopanda jukwaani leo ni pamoja na Pendo
Laiser, Lisa Jensen, Christine Willium, Jenifer Kakolaki, Gloryblanca
Mayowa, Hamis Hasan, Queen Saleh, Mwajabu Juma, Neema Saleh na Stela
Mbuge.