MADRID,Hispania
WINGA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amesema
hafikirii kuondoka klabu hiyo ya Hispania na badala yake angependa kuona
anamaliza jukumu la kucheza soka hapo hasa baada ya kuiwezesha klabu
hiyo kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania.
Ronaldo (27),
aliyeweka rekodi ya uhamisho ya pauni 80 milioni (Sh191 bilioni) akitoka
klabu ya Manchester United ya England, amefunga mabao 46 ligi kuu msimu
uliopita na kumaliza utawala wa Barcelona uliodumu kwa miaka minne.
"Kama
uamuzi ungekuwa wangu, basi ningependa kubaki Real Madrid mpaka
nitakapostaafu soka, ni kweli kabisa," alisema Ronaldo."Leo hii
ningekuwa tayari hata kusaini miaka 10 kubaki hapa, lakini uamuzi kama
huu unategemea pia watu wengine."
Ronaldo, aliyefunga mabao 55
katika mechi 60 za mashindano msimu uliopita, alikiri kwamba ana hamu ya
kurejesha kile alichofanyiwa na klabu hiyo kwa kumpa dau kubwa la
uhamisho.Aliongeza: "Yote niliyofanya, nimefanya kwa jasho langu na
kipaji, lakini hakuna litakalopotea angani."Kwa sasa naendelea kubaki
mchezaji niliyehamishwa kwa ada kubwa, na siku zote nimekuwa nikijaribu
kuthibitisha hilo uwanjani," alisema.
Ronaldo, ni sehemu ya kikosi
cha Ureno kinachojiandaa na michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya na
amefurahishwa kuona kocha wake, Jose Mourinho amesaini mkataba tena na
Madrid mpaka mwaka 2016.
Katika mahojiano na gazeti la Hispania, Marca, alisema: "Nimefurahi kuona Mourinho akibaki.
"Klabu
kama Real Madrid inapaswa kuwa na kocha mzuri kama [Jose]Mourinho.Kocha
ameamua kubaki, na kwangu naamini Real Madrid haiwezi kutwaa Kombe bila
Mourinho kuliko kama angekuwapo kwenye benchi."