MENU

Thursday, June 21, 2012

Ajali yaua sita Dar

Watu wapatao sita wanahofiwa kufa katika ajali iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Tegeta Kibaoni baada ya gari aina ya Scania lililokuwa likitokea kiwanda cha Saruji cha Wazo Hill kupata hitilafu ya breki na kugonga daladala aina ya Isusu Journey kisha kuangukia watu waliokuwemo kwenye Baa ya KMM.